Je, nikikata bima yenu nitatibiwa magonjwa yote?
Ukiwa na bima ya Jubilee utatibiwa magonjwa mengi, lakini kuna magonjwa ambayo hayapo katika bima ambayo yameainishwa katika hati ya sera utakayopewa kabla ya kujiunga. Pia kuna magonjwa ambayo yana muda wa kusubiria wa mwaka mmoja mpaka miaka miwili kama vile kisukari, magonjwa ya moyo, shinikizo la damu, kansa, HIV na kadhalika, pia utapewa hati inayoonyesha magonjwa hayo na muda husika wa kusubiria.